Wednesday, 15 January 2020

Kuhusu Akiba .(Kiuchumi)

Mkakati no 1.(Kiuchumi) 
Jifunze kuweka akiba ya Kifedha kila mwezi  na Kuilinda.
Usipoweka Akiba wakati Mungu anakubarikia au amekubarikia ni Dhahiri pia miaka saba ijayo  (Asomaye na Afahamu)unajitengenezea mazingira ya kuuza hata ulivyo navyo vya Thamani kwa bei ya Hasara...
Neno .1Timotheo 6:17-19.
Pigia mstari Verse No.19
Huku mkijiwekea AKIBA, iwe msingi mzuri kwa wakati UJAO.

Mkakati 2. 
Hakikisha Akiba ya Kifedha Unayoweka inakuwa na Utaratibu maalumu wa kimkakati katika Kiuwekezaji ili kufikia au kutimiza malengo kusudiwa KIUWEKEZAJI
Naamisha weka akiba kulingana na Count Cost ya Project au Biashara unayotaka Kufanya, au weka akiba Kimalengo.. (Kama kwa mwaka unataka Return on Invest iwe 1,000,000, kulingana na kipato chako  basi ni dhahiri uwe na kiwango cha Kuanzia kuweka akiba kila mwezi)
Usiweke akiba isiyokuwa na Malengo HAUTAILINDA!
(1Nyk 29:16,19)Akiba Kimalengo

Mkakati no 3.
Hakikisha unamuomba Mungu ndani ya Moyo wako Akuweke Moyo Mkamilifu ili uwe na Hekima ya Kitumia Akiba katika Malengo Mahususi na Sio Vinginevyo.
Daudi alimwombea Mwanae Awe na Moyo Mkamlifu na Hekima ili Kufuata maelekezo ya Mungu pamoja na Kuijenga Nyumba (Kama pRoject kwake au katika Ufalme wake)aliyoiwekea AKIBA.
Note:AKIBA SIO FEDHA ZA ZIADA AU VITU VYA ZIADA IJAPOKUWA INAWEKA IKAINGIA KAYIKA HALI YA AKIBA
AKIBA NI MPANGO MKAKATI WA VITU INAVYOPATA ILI vikufae kwa wakati Ujao
  
Mkakati No.4
Akiba Inabeba maelekezo, USIWEKE AKIBA BILA MAELEKEZO KIMAANDISHI.
DAUDI aliweka Akiba kwa ajili ya Kujenga Nyumba ya Bwana, Lakini Akiba Hiyo ilimfanya aachilie maelekezo ya Kimungu kwa Mwanae Suleiman.
1Nkt 22:3,5,14
Asomaye na Afahamu.
Mwisho.
Kwa uchache ulionao, unaweka ukaweka akiba kabisa, Cha Msingi Weka akiba Kimalengo na Iwe yenye Kukupa Faida, Kumbuka katika SHIDA Daudi aliweka akiba kwa lengo la KUJENGA NYUMBA YA BWANA (1Nyk 22:14)
Na Muombe Mungu akufundishe ili Uone faida na kuipata.
Isaya 48:17
Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata

Utaratibu wa Kimalengo katika uwekaji wa Akiba:
  • Rule 1.
Jifunze au Jizoeshe kuweka akiba ya Kifedha kwa Kila mafanikio yako au unachopata kwa jinsi ya Thamani ya Fedha, Walau katika Wiki, Mara Moja na katika Mwezi Mara Nne Kithamani.kama unaweka 40000 kwa wiki, unawekeza 120000 kwa mwezi katika Ujumla wake.
Mwnzo 41:36
Kwa kile walichokipata waliweka akiba yao kwa malengo yaliyofungwa kwa miaka 7
  • Rule 2.
Jifunze kugeuza akiba unayoweka kama "Nafaka" ili iwe "Chakula" kwa ajili ya baadae..
Akiba huchakatwa kimalengo ili kugeuza akiba hiyoniwe yenye kufaa au thamani njema hapo baadae, Usiweke Akiba Nje ya Malengo uliyonayo, Akiba kimalengo yanakupa Msuli wa kuchakata akiba kuwa Chakula.
Mwanzo 41:35 pigia mstari "Akiba ya Nafaka"
Asomaye na Afahamu
  • Rule 3.
Jifunze kuweka akiba kwa jinsi ya Wakati uliokusudiwa kimalengo,
Ifanye sehemu ya akiba yako mara baada ya muda fulani IZAE AU IONGEZEKE kwa sababu kila akiba imebeba Nyakati zilizokusudiwa.
1Samweli 9:23 "lete ile sehemu nliyokupa, hiyo (alichopewa)niliyokuambia ,IWEKA AKIBA
(Sehemu ya Akiba katika Akiba kwa wakati uliokusudiwa -1Sam 9:24)
  • Rule 4.
Epuka kutumia akiba uliyoweka kabla ya muda wake, na kinyume na malengo ndani ya akiba na nje ya muda uliokusudiwa. 
Kila akiba Kimalengo imebeba Kusudio, muda uliokusudiwa na utekelezaji wa kimalengo.
Ukitumia kabla ya muda ni dhahiri ya kuwa akiba yako ipo nje ya muda wa kimalengo uliokusudiwa.
 Mungu Akubariki Sana

NADHIRI

MAOMBI YA NADHIRI YAAMBATANAYO NA SADAKA YA NADHIRI NENO; Mhubiri 5:4 “ wewe ukimwekea Mungu nadhiri ,usikawie kuiondoa” Maombi...