Msingi wa nne
Thamini ulichonacho kwanza kwa jinsi
ya Mungu ukiamini kuwa akupaye hicho ni Yeye ili ujue namna gani
utakitathaminisha hicho ulicho nacho kama thamani ya kukiongezea thamani yake
ili usiwe mwepesi kuishia njiani
Kwa sababu “aliye nacho atapewa
zaidi(aliye ona uthamani wa hicho kidogo alicho nacho kitathaminisha hicho na
kuongeza thamani) na asiye nacho , na hata hicho kidogo alicho nacho
atanyang’anywa( asiye ona thamani ya alichonacho, hata akitaka kukizalisha
alicho nacho itafikia sehemu atakwama tu kama sio kuishiwa kabisa) Mrk 4:25
Linganisha na hapa “Ukiwa mwaminifu
kwa hicho kidogo ulicho nacho au ulicho kianzisha basi ni rahisi sana kuwa
navyo vingi na kwa sababu hiyo uaminifu wako hukufanya uwe msimamizi kwa hivyo
vingi utakavyo pata ,kinyume chake usipokuwa mwaminifu kwa hicho ulichonacho si
rahisi kuweka matumaini ya kuapata zaidi ya hicho ulicho nacho na ifikapo
wakati wa taabu utakwama hakika na
kuvunjika (Mithali25:19)
Cheki
Mtu mwaminifu atakuwa na Baraka(guvu ya kufanya vitu na kumaliza na
kukupa utajiri tele, kumbu 8:17-18) tele (mithali 28:20a)
Thamini mbegu uliyo nayo ndani kwa
itakupa thamani ya kuithaminisha kiutekelezaji ili ikupe matokeo kulingana na
Thamani uliyoiweka kwenye mbegu kwa kumuhusisha Mungu, kwa sabau wazo la
kukufanikisha linatoka kwa Mungu
Kwa kuwa Mbegu yako Mungu huipa
mwili(matunda) kama apendavo (1Kor 15:37-38) na apandaye si kitu wala atiaye
maji ila Mungu akuzaye, Maana sisi hufanya kazi pamoja na Mungu (1Kor 3:7-9)
Msingi wa tano
Jua aina ya watu wa kuhusiana nao wakiwa rafiki kama kweli wamebeba
jambo la kujifunza kutoka kwao kulingana na jambo ulilonalo nalo ili mara
nyingine ulichojifunza kikutie moyo na kukupa nguvu ya ksonga mbele pale
unapokwama
Yesu alifikia sehemu akiwa na huzuni sana na kufadhaika kutokana na
ugumu wa kazi ya msalaba mbele, akawachukua akina Petro, Yakobo na Yohana
wakakaa pamoja naye wampe company ya kuomba, lakini walikuwa wamelala (Mrk
14:33-38)
Sasa cheki kama ulio nao wana uwezo wa kushikamana na wewe katika kila
hali kwenye hilo jambo maana wengine watalala njiani na kukuacha mwenyewe
Cheki kama wana “Stamina” ndani yao ya kuikabili changamoto utakayo
kutana nayo na kukutia moyo ili usonge mbele
Lakini, jifunze kutokuwa mtegemezi kwao ili kufanikisha jambo au kazi
iliyoko mbele yako, si kila rafiki uliye naye ni rafiki mwenye msaada kwako,
wengine ni wataabishaji(Ayubu 16:2-3)
Lakini pia ona furaha ya Bwana kwenye hilo jambo kwa namna ya
kukufanikisha, maana Furaha ya Bwana ikakuja na NGUVU YA KUMALIZA JAMBO(Nehemia
8:10)
Msingi wa sita
Jifunze kumpa Mungu nafasi yake kwa
kuwa yeye aliyekupa wazo,namna ya kutekeleza ndiye atakayeikamilisha njio hiyo
ya utekelezaji
Ukitaka kuwa mkamilifu katika
utendaji wa jambo na lifanikiwe, kubali na fahamu kuwa kila wazo jema
lililobeba mafanikio yako kiutekelezaji ni la Mungu,
Tazama hapa,
Mt 17:24-27
Yesu alimpa Petro “Njia ya utekelezaji wa kuapata fedha uliofichwa
kwenye wazo la kwenda Kuvua samaki azukaye wa Kwanza(sasa utaelewa atoaye wazo
ni Mungu, nay eye ndiye mwenye kuisimamia katika utekelezaji) na akifumbua
mdomo wake Petro ataona shekeli, alafu akamlipie kodi yake na Petro”
Sasa unaweza ukaelewa kuwa “Petro asinge tii na kumpa Yesu nafasi
asingepata wazo”
Na kwa sababu hiyo angekuwa bado ana
deni la shekeli,
Sasa ,kama Yesu anakupa wazo ndani
yako, na namna ya kulitekeleza jifunze kutii na kumpa nafasi, lakini pia Mpe
asilimia 50% ya kwake kwa kila tunda litakalopatikana ndani ya huo utekelezaji
wa jambo lake ili usije ukakwama njiani mara uanpotekeleza jambo hilo liwe
endelevu kwenye maisha yako
Swali,
Sasa utajuaje hili jambo likifanikiwa lazima nimpe Yesu 50% ili
nisikwame hapo badaye ndani ya wazo hilo hilo kiutekelezaji?
Jibu
Cheki mazingira ya upatikanaji wa wazo na namna ya kulitekeleza na
angalia matunda yake baada ya kulifanyia kazi
Cheki changamoto uanzokutana nazo na pima kama akili zako zinaweza
zikakupa majibu ya kujua namna ya kutatua changamoto hiyo
Cheki utafauti wa wazo na aina ya watu ulioko nao kama wana wazo
linaloendana na la kwako na pima matunda unyoapata kama ni ya samaki wa
kwanza(nikimaanisha linganisha mbegu yako na matokeo ya mbeguna hali ya
kufanikiwa kwenye eneo lile)
Naamini hizi dondoo chache zitakupa
kitu cha kukusaidia, Mungu akubariki sana
kupata misingi iliyopita Bofya hapa
Msingi wa tatu
kupata misingi iliyopita Bofya hapa
Msingi wa tatu