Monday, 4 December 2017

MISINGI KADHAA YA KUKUPA UFAHAMU ANGALAU UJUE NAMNA YA KUMALIZIA JAMBO ULILONALO AU WAZO LILILOKO NDANI YAKO KWA NAMNA YA KIMUNGU



Msingi wa tatu

    Kuwa na maarifa ya kutosha kuhusiana na hilo jambo ambalo unalianzisha kwa kuona matokeo (archievements) ili kukusukuma zaidi katika kuongeza ufahamu katika jambo hilo
“kimatokeo, utajifunza uthamani wa hilo jambo na ukubwa wake na kukupa akili yenye akili ya namna ya kulikamilisha”
Isaya 46:10 “Nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale..shauri langu litasimama, name nitatenda mapenzi yangu yote”
      Kwenye maarifa(siri ndani ya neno) kuna mwanga (Ufahamu), kuwa na wazo ni mbegu, usipojua namna ya kuipanda mbegu, wapi na udongo gani na majira gani na wakati gani na usipojua matokea ya mbegu kama chakula kwa kiwango gani ni rahisi sana kuishia njiani(Zab 119:105)
      Kwa sababu “Ufahamu mwema huleta  upendeleo” na moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa na ufahamu ni chemichemi ya UZIMA  kwake yeye aliye nao(Mithali 13:15a,15:14a,16:22a)
    Kumbuka pia ukiwa na ufahamu kwa kiwango stahiki ni lazima jambo lako lidhibitike hakika (mithali 24:3)
Tazama mfano huu
        Mpanzi (Mwenye mradi wa kimaendeleo) alikuwa na mbegu(wazo la kuzaa jambo la kumfanikisha) na mbegu hiyo akafanya kwanza uchunguzi kwa kuiweka katika makundi manne lakini kundi moja tu lilimzalia  matunda bora na mema  na kuona faida ya mbegu hiyo)kwa hiyo
Unaweza ukawa na wazo kama mbegu ndani yako na ukawa una ufahamu wa eneo moja lazima ukwame
Unaweza ukawa na mbegu lakini ukawa mvivu wa kutafuta aina tofauti tofauti ya ufahamu wa mbegu uliyo nayo kwa sababu hiyo lazima uishie njiani tuu
Unaweza ukawa na mbegu (wazo)usione umihmu wa mbegu hiyo na ukashindwa kujua aina ya udongo wa kupanda mbegu yako na kwa sababu hiyo utaishia njiani na wazo lako
Unaweza ukawa na mbegu na ukawa na ukakosa ufahamu wa mahala sahihi pa kupanda mbegu , kwa hiyo utakwama tuu njiani

Swali,
    Jee kwa nini mbegu hiyo hiyo ya aina moja iliwekwa kwenye maeneo manne tofauti na sehemu moja tu mbegu lizaa matunda? (Mt 13:3-8)
    Kuwa na ufahamu wa kutosha na chanzo zaidi ya kimoja cha maarifa kuhusu jambo lako itakusidia kuafanya “visibility study” na kukupa maarifa zaidi ya namna na wapi pa kupanda mbegu yako na kukufanikisha
     (Pilot study imejaa maarifa ya namna ya kufanikisha jambo bila kukwama, na Pilot study ipo kwa watu sahihi wa namna yako wale waliokutangulia sio kwa kuiga ila kwa kutafuta maarifa, kuiga kwingi hukwamisha watu)
kupata Misingi iliyopita bofya hapa
Msingi wa kwanza
Msingi wa pili

itaendelea msingi wa nne..
MUNGU AKUBARIKI SANA

NADHIRI

MAOMBI YA NADHIRI YAAMBATANAYO NA SADAKA YA NADHIRI NENO; Mhubiri 5:4 “ wewe ukimwekea Mungu nadhiri ,usikawie kuiondoa” Maombi...