Saturday, 2 August 2014

NAMNA MADHABAHU ZINAVYOWEZA KUSHIKILIA MFUMO WAKO WA MAISHA



NAMNA MADHABAHU ZINAVYOWEZA KUSHIKILIA MFUMO WAKO WA MAISHA
NENO :Waamuzi 6:24
Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri.”
Madhabahu ni eneo ambalo linaweza kutumia na Mungu au shetani ili lijengwe kwa kupitisha nguvu ,mamlaka na utawala wake na kila madhabahu ina tabia zake.
Madhabahu ni eneo ambalo linakuwa daraja kutoka ulimwengu war oho kupitisha kilichokusudiwa  hadi ulimwengu wa mwili au nyama.NAmadhabahu  zinatenda kazi kulingana na utawala na mfumo wa mmiliki wao.au kwa  lugha nyingine madhabahu ni  eneo litumiwalo na watu watu Fulani kwa ajili ya kufanya ibada zao wakiwa na imani ya nguvu  ya pale,mungu wa eneo lile kulingana na utaratibu wa lile eneo na kila madhabahu zinategemea na utendaji wa roho wa eneo lile au miungu wa madhabahu husika.Zipo madhabahu za aina mbili au zenye utawala wa namna mbili,
         A)Madhabahu ya MUNGU.
         B)Madhabahu ya shetani.
Ili hizi madhabahu zifanye kazi zinategemea sana
Ø Mungu wa madhabahu
Ø Nguvu ya madhabahu
Ø Sadaka zitolewazo madahahu husika
Ø Nguvu ya kuhani husika
Sadaka zitolewazo katika madhabahu husika  zinauhusianao mkubwa sana na nguvu itokayo katika madhabau husika juu ya mfumo husika wa maisha yako na maono uliyobeba juu ya maisha yako ya badae.Na madhabahu ya MUNGU au ya shetani zote zinafanya kazi kulingana na ene lililopo katika ulimwengu wa roho yani kulingana na itifaki ya kiutawala juu ya madhabafu husika au mahali pa juu husika katika ulimwengu war oho.(Yeremia 32.35 “Tena walijenga mahali palipoinuka kwa Baali, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kuwapitisha wana wao na binti zao katika moto kwa ajili ya Moleki, jambo nisilowaagiza; wala halikuingia moyoni mwangu kwamba walitende chukizo hilo; wapate kumkosesha Yuda”)
(Waamuzi 6;26 “ukamjengee Bwana, Mungu wako, madhabahu juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; ukamtwae yule ng'ombe wa pili na kumtoa awe sadaka ya kuteketezwa, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata
Kwa hiyo kila mabdhabahu inataratibu zake na sadaka zake na ina toa matokeo kulingana na sadaka zitolewazo katika madhabahu husika.ANGALIZO. “NGUVU YA MADHABAHU HUTEGEMEA SANA KIWANGO CHA SADAKA ITOLEWAYO KATIKA MADHABAHU HIYO.”Matendo:10;2-4 Kornelio alikuwa amebeba madhabahu ya Mungu na sadaka zake zilisababisha nguvu za Mungu katika madhabahu ya Munguiliyokuwa  ndani yake zitoe majibu ya maombi yake ya Muda mrefu mbele za Mungu,,ulishawahi kujiuliza kama angekata tamaa kutoa sadaka nyingi ingekuwaje? “Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.
  Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro.”hii ina maana kuwa sala zako ziambatanazo na sadaka katika madhabahu yangu zimefika kikamilifu na sasa majibu ya maombi yako yanatoaka mahali pangu pa juu..(madhabahu ya Mungu)
Hivyo basi nguvu ya madhabahu kukupa majawabu ya maombi yako inategemeana sana na sadaka unazotoa katika madhabahu.Madhabahu ni daraja kati yako inayopitisha vitu kati yako na Mungu unayemtumkia.Swali la kujiuliza jee unajua upo katika madhabahu gani hata kama umeokoka? yawezekana hata kama umeokoka bado umevaa Sanda (nguvu ya madhabahu Fulani)Maana haikutosha tu kufufuliwa kwa Lazaro na Yesu mpaka ilipotolewa amri ya kumvua sanda..haitoshi ya kuwa wewe tayari unatiketi ya kwenda mbinguni,,,Je mfumo wa maono uliyobeba yanakwendaje..vipi elimu ipo sawa sawa..maendeleo yako ya kiuchumi yapo sawasawa..suala la ndoa jee limekaa sawasawa?(Yohana 11.43-44)
Ngoja kushirikishe hili,SADAKA YA MADHABAHU

Kiitifaki sadaka zitolewazo madhabahu Fulani huwa zinahuisha na kutiisha nguvu ya madhabahu hiyo.Kama upo katika madhabahu ya Mungu aliye hai unaambatanishwa na vitu vitano  ambavyo ndani yake kuna  mfumo mzima wa kiiutawala juu ya maisha yako na maono uliyonayo.Unaambatanishwa na,
Ø Mungu wa madhabahu
Ø Nguvu ya madhabahu
Ø Sadaka za madhabahu
Ø Ibada za eneo hilo
Ø Na kuhani wa madhabahu hiyo.
Ukisoma mwanzo 8;,20-22.” Nuhu akamjengea Bwana madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
 Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, maana mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya.
 Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma.”utaona kabisa Sadaka aliyoagizwa Nuhu atoe zinaachilia mfumo mpya wa maisha yao na ndani yake kuna ibada,sadaka,nguvu ya madhabahu,kuhani na Mungu mwenyewe.
Madhabahu zote huanzishwa katika ulimwengu war oho na utendaji wake kuwepo katika ulimwengu wa kawaida au wa nyama.
Madhabahu zinatoa maelekezo ya mfumo wa maisha yako kwa kujua au kutokujua ndio maana yapo makabila mengi hapa Tanzania ambayo yana muda maalumu wa kutoa sadaka ila mambo yao yaendea sawia,we unafikiri ni hali ya kawaida la hasha!Mfumo wako wa maisha umefungwa kwenye madhabahu.
Madhabahu ya ulimwengu war oho huunganishwa na madhabahu za ulimwengu wa nyama kupitia
v Sadaka
v Makuhani
v Ibada zifanyikavyo kwa wakati.

MAMBO YAKUUNGANISHAYO NA MADHABAHU HUSIKA.
(1)Jambo la kwanza;SADAKA.
Sadaka ni njia mojawapo ya kuunganisha maisha yako mwenyewe na wewe mwenyewe na vizazi vyako katika madhabahu husika ndio maana Yesu alifanyika sadaka ili tuwe na mamlaka na ukuhani katika Ufalme wa Mungu Ebrania :28” na kadhalika Kristo naye, akiisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi; atatokea mara ya pili, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu
Chunguza katiaka ukoo wako kabila ni muda gani wanatoa sadaka na kwa sababu gani?Uthamani wa sadaka ndio nguvu ya miungu ya madhabahu husika.Waamuzi 6:25-32 Gideoni alitoa sadaka ili kuwatoa wana wa Israeli katika miungu Baali na kuwaunganisha na madhabahu ya MUNGU pasipo wao kujua ndio maana inaleta shida mara baada ya kugundua  mungu wa baali hayupo.Na kila sadaka inautaratibu wake kulingana na nini na kitu gani kinakusudiwa kitokee ndio maana ukienda kwa waganga wa uchawi wana aina tofauti tofauti ya sadaka kutokana na matokeo unayoyahitaji,kadhalika  kila madhabahu ina mungu wake na mfumo wake.
Ukisoma Waamuzi 6:29-30 Wakaambiana, Ni nani aliyetenda jambo hili? Hata walipotafuta habari na kuuliza, wakasema, Gideoni, mwana wa Yoashi, ndiye aliyetenda jambo hili.Ndipo watu wa mji wakamwambia Yoashi Mlete mwanao, afe; kwa sababu ameibomoa madhabahu ya Baali na kwa sababu ameikata ile Ashera iliyokuwa karibu nayo Angalia kuitoa madhabahu ya baali ilisababisha ugomvi juu yao kwa sababu “ameikata”maana yake amewatenga na miungu baali ya kwao na kuwaunganisha na MUNGU aliye hai.Mifumo ya kiutawala ya kwao ilitawaliwa na Miungu migeni ndio maana kila mtawala wa wakati ule Israeli alijiunganisha na miungu baali.
Maisha yako namna yalivyo inawezekana kabisa ulifungwa kwenye sadaka na kutolewa kwenye madhabahu Fulani,we chunguza habari ya maisha mlionayo.Unaweza ukaingizwa kwenye mungu wa madhabahu fualani pasipo wewe kujua badala yake utaona mabadiliko katika mfumo wa maisha yako.”Kuondolewa kwa madhabahu ya baali iliinua vita vingine si kwa sababu madhabahu iliondolewa la hasha,bali mfumo wa maisha ya kiutawala juu ya Israeli umebadilishwa Ezra 3:3 Hata ulipowadia mwezi wa saba, na wana wa Israeli walipokuwa katika miji yao, watu wakakusanyika pamoja huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
 Ndipo akasimama Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zake makuhani, na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na ndugu zake, nao wakaijenga madhabahu ya Mungu wa Israeli, ili  kutoa sadaka za kuteketezwa juu yake, kama ilivyoandikwa katika torati ya Musa, mtu wa Mungu.
 Wakaiweka madhabahu juu ya msingi wake; maana hofu imewashika kwa sababu ya watu wa nchi; wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu yake, sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni.Mfumo wa maisha ya Israeli ilisababisha watoe sadaka itakayowaunganisha na Mungu aliye hai ndio maana wakakusanyika pamoja   Je upo kwenye madhabahu gani inayoamua maisha yako?

(2)Jambo la pili:Majina uliyopewa yanaweza kabisa kukuunganisha na miungu wa madhabahu Fulani.wengi wana majina lakini hawajui asili ya majina yao.
Palipo na jina hapo ndipo kuna utambulisho wa mtu katika vision yake na mfumo mzima wa maisha yako.Adamu alipewa mamlaka ya kuwapa majina viumbe walioumbwa na Mungu kwa nini,sababu moja wapo utambulisho wao katoka ulimwengu war oho upo kwenye majina.kadhaliaka future yako inauhusiano mkubwa sana na jina ulilonanlo sasa.Jamii nyingi hapa wanatabia ya kurithishana majina  wakiamini mhisika bado yupo  na hapo ndipo unapounganishwa na miungu ya kikabila na kiukoo na mfumo wako wa maisha utakuwa chini ya madhabahu hizo za kiukoo,na maono yako yamefichwa huko hata kama umeokoka (mwenye maarifa na afahamu)Mwanzo 2:19-20. Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake.
  Adamu akawapa majina yao kila   mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye.
Yakobo nae alibadilishwa utambulisho wake na kuitwa Israeli maana yake mbarikiwa na Ibrahimu pia kwa nini? Future ya mtu ina uhusiano mkubwa na jina la mtu,kadhalika na madhabahu zinahusika kabisa na mfumo wote wa maisha ya mtu hivyo jina ulilonalo yatosha kabisa kuunganishwa na miungu wa madhabahu husika.Angalia baada ya Abraham kuitwa Ibrahimu  Mungu anamwambia maana ya jina lake,,yaani limebeba nini hapo badae,Mwanzo 17:6-8
Hivyo madhabahu Fulani inatambua vision yako hapo baadae na kwa kuwa ni chanzo au eneo ambalo linatawala mfumo mzima wa maisha yako hapo badae basi jina lako linaweza likaunganishwa na madhabahu fualani.Ndio maana kila jina lina maana si kawaida ila ni utambulisho wa roho iliyoko kwenye majina Jina lako au maana ya uhai wako upo kwenye nafsi na nafsi imebeba uhai wako(Roho Mtakatifu akufunulie hili jambo)nafsi ikifa uhai wako haupo,kadhalika miungu ya giza hushughulika sana na nafsi ya mtu kama ndivyo utambulisho wako upo ndani ya nafsi na nafsi imeficha jina lako hapo,Basi jina lako ni njia mojawapo ya kuunganishwa na madhabahu husika.
(3)jambo la tatu.Maagano yaliyowekwa mwanzoni yatosha kukuunganisha na madhabahu za giza Je kuna maagano mangapi nay a aina gani ambayo wazazi wako waliweka wakati unazaliwa aidha kupitia kitovu au damu yako au nywele zako,zilifungwa kwenye miungu gani?si suala la kujiuliza mpendwa. Yapo maagano ya aina nyingi,lakini agano la damu ni agano lenye nguvu kwa sababu damu ina sauti,uhai,na damu inatoa laana,Ebra,12:24,Lawi 17;10-12.Kumbuka yapo maagano ya Damu yaambatanayo na sadaka kwa ajili ya ibada za miungu migeni.
Hivyo damu pia inahusika kabisa katika kuamua maisha yako ya badae kulingana na maagano yaliyoko katika damu na wewe.Ndio maana wachawi nao hupenda sana kutumia damu kwa ajili ya kukamata mfumo wa maisha ya mtu ,nafsi katika madhabahu zao.
Madhabahu nyingi zinakuwa na Nguvu kutokana na maagano ya damu.Angalia nabii Eliya alivyounganisha kabila 12 za majina katika Israeli na damu pia.hivyo damu inatosha kabisa kukuunganisha na madhabahu Fulani.(1Wafamle 18:32-35 Naye akaijenga madhabahu kwa mawe hayo katika jina la Bwana; akafanya mfereji, kama wa vipimo viwili vya mbegu, ukiizunguka madhabahu.
  Kisha akazipanga zile kuni, akamkata yule ng'ombe vipande vipande, akaviweka juu ya kuni. Akasema, Jazeni mapipa manne maji, mkayamwage juu ya sadaka ya kuteketezwa, na juu ya kuni.
  Akasema, Fanyeni mara ya pili. Wakafanya mara ya pili. Akasema, Fanyeni mara ya tatu. Wakafanya mara ya tatu.
 Yale maji yakaizunguka madhabahu; akaujaza mfereji maji.)Eliya alifanya hivyo kulingana na uhusika wa madhabahu,na majina Damu na sadaka Mapipa manne,pande nne za Israeli,wakajaza maji na kumwaga juu ya juu ya sadaka ya kuteketezwa,mara tatu hesabu yake ni 12 saw na akbila 12 za Israeli kutoka pande nne za dunia,kiroho maji damu zinashuhudia hapa duniani (1Yoh 5:9) na ndani ya sadaka kuna damu na maji na majina ya isreali KIKABILA juu ya madhabahu,kwa mantiki hiyo Majina ya Israeli yalifungwa kwenye madhabahu na sadaka zake na katika sadaka kuna Damu iliyomwagia katika hiyo madhabahu ya MUNGU.
Watu wengi mfumo wao wa kimaisha unayumba kutokana na maagano ya damu yaliyowekwa kwenye madhabahu husika ambayo yamefunga maisha yao katika madhabahu za miungu yao.Wengi huenda hawajua yakupasa ujue utaratibu wa ukoo wenu na historia ya ukoo wako ili ujue namna ya kutoka huko.Binafsi ilinigharimu miaka miwili ya maombi kuombea maagano na familia yangu kiujumla kwa uwezo wa Roho  Mtakatifu.
Tazama name kipindi cha Nuhu,mara baada ya gharika jambo la  kwanza Nuhu kufanya ni kumjengea Mungu madhabahu ili mfumo mpya wa kizazi kilichobakia uwe ndani ya madhabahu ya Mungu(Mwanzo 8:20-22. Nuhu akamjengea Bwana madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
  Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, maana mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya.
  Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma.Mungu atasema Baraka juu ya maisha yao na majira na nyakati  katika mfumo mpya wa maisha,yote hayo ni baada ya kutoa sadaka ya damu juu ya madhabahu ya Mungu(akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.) Mungu anasema “Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, maana mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya.”maana yake anaachilia Baraka katika mfumo mpya wa maisha yao.
Madhabahu zimekamata mfumo mzima wa utawala wa  maisha ya mtu.

(4)Jambo la nne;Viapo vya wakuu wa makabila na miungu yao yatosha kabisa  kukuunganisha na madhabahu baali,Hii pia ni njia mojawapo ya kukuunganisha na miungu ya kigeni ukisoma Habakuki 3:9” Uta wako ukafanywa wazi kabisa; Viapo walivyopewa kabila vilikuwa neno thabiti; Ukaipasua nchi kwa mito”utaona kuwa kuna viapo  tosha kabisa juu ya kabila na vina uthabiti ju ya mfumo wako wa badae.
Angalia Amosi 1;6-8 kufungwa kwa kabila ni juu ya maaganao au viapo wa miungu yao ya kikabila ndio maana huenda maisha yako yamefungwa kwenye madhabahu ya kiakabila.
-          Chunguza vizuri katika Amosi 1:6-8 – Hapo unaona kabila zima limepigwa pingu na kufungwa kisha kutiwa katika mikono ya Edomu (roho ya kuhangaika na kufa vibaya) nguvu hiyo ya kulifunga kabila zima ilitoka kwenye kati ya miji ile 5 ya wakuu wa Wafilisti (wakuu wa giza) waliokuwa wanatawala miji mitano ya wafilist. Kwa hiyo kabila zima lilifungwa kwa upako wa giza ulioachiliwa kutoka kwenye miji 4 ya wakuu wa giza – yaani, Gaza, Ashdodi na Ashkeloni pamoja na Ekroni.
miungu iliweza kulifunga kabila zima. Je! Iliwezekanaje kukamata kabila lote na kulifunga? Kwa kupitia mtu mmoja (mkuu wa kabila) miungu ikalifunga kabila.
Wakuu wa giza hushughulika sana na wakuu wa makabila na Mungu nae hushughulika pia na wakuu wa kabila waliobeba kabila Fulani.Angalia vipaumbele vya kabila 12  za Israeli.
Mwanzo 49;3-4 Reubeni, u mzaliwa wangu wa kwanza, Nguvu zangu, na malimbuko ya uwezo wangu. Umewapita wengine kwa ukuu na kwa nguvu.
 Umeruka mpaka kama maji, basi usiwe na ukuu, Kwa sababu ulikipanda kitanda cha baba yako, Ukakitia unajisi; alikipandia kitanda change Reuben alipozini na mke wa babaye iliharibu hatima ya kizazi chake ,nachotaka ujue Mungu huangalia waanzilishi wa kabila na si watakaofuata…mfumo wa badae wa kizazi cha Reuben uliharibika kutokana na Reuben mkuu wa kabila la Reuben.
Leo hii hayo mambo yapo hiyo ni madhabahu ya uasherati iliyowekwa na waanzilishi wa kabila lako,huenda kuna mambo ambayo hujapata ufumbuzi mpaka sasa fuatilia habari ya kabila lako na viapo vyao.Reubeni alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza lakini Baraka zote alipewa Yusuph nduguye,vipo viapo vingi vya kabila lako ambavyo vilikuunganisha na madhabahu ya baali na mpaka sasa inashughulika na maisha ya vizazi vyako mpka Mungu mwenyewe aingiie kati.(1Nyakati 5:1-3. Na wana wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli; (kwa maana ndiye aliyekuwa mzaliwa wa kwanza, lakini, kwa kuwa alikinajisi kitanda cha babaye, haki yake ya mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yusufu, mwana wa Israeli; tena nasaba isihesabiwe kwa kuifuata hiyo haki ya mzaliwa wa kwanza.)
 Kwani Yuda ndiye aliyeshinda miongoni mwa nduguze, na kwake ndiko alikotoka mtawala; bali haki  ile ya mzaliwa wa kwanza alipewa Yusufu);

(5)Jambo la tano.Kuingia katika eneo ambalo wanaabudu miungu mingine yatosha kukuunganisha na madhabahu zao
.Waamuzi 2;11-13 Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya Bwana, nao wakawatumikia Mabaali.
  Wakamwacha Bwana, Mungu wa  baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika.
  Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi.Kama umeokoka na hauna stamina ya kiimani katika Kristo ndani yako na nguvu ya Roho Mtakatifu ni rahisi sana kuruhusu madhabahu nyingine iingilie na kutawala mfumo wa maisha yako ya kiroho.Inategemea sana na nguvu ya Mungu itendayo kazi ndani yako binafsi au upako wa Mungu juu yako binafsi.
Wana wa Israel waliingia kwenye miungu ya kigeni kutokana na upako wa viongozi wao ndio maana walipoachwa walianza kuabudu miungu migeni ya madhabahu za kigeni.fuatilia tangu walipoanza safari  toka Misri,kukaa kwao kiimani kulitegemea sana na imani na uimara wa kiongozi waona si wao wenyewe haijalishi waiweka maagano ya namna gani na Mungu na kwa kiwango gani.,
(6)jambo la sita.Kujiingiza kwenye agano la ndoa unaachilia mfumo mpya wa utendaji kazi ndani yako.Unapoingia kwenye suala zima la ndoa yapo mambo ya msingi sana ya rohono yakupasa ushughulikie  kabla ya ndoa ili imani yako katika Kristo Yesu iwe thabiti.maana unapoingia kwenye ndoa ni agano lingine la kiamisha kwako na lina uhusiano mkubwa sana na maisha yako ya kiroho.Waamuzi 3;4-7 Naye aliwaacha ili awajaribu Israeli kwa hao, apate kujua kwamba watasikiliza amri za Bwana, alizowaamuru baba zao, kwa mkono wa Musa.
 Basi wana wa Israeli wakaketi kati ya Wakanaani; hao Wahiti, na hao Waamori, na hao Waperizi, na hao Wahivi na hao Wayebusi;
 wakawaoa binti zao, na binti zao wenyewe wakawaoza wana wao waume, na kuitumikia miungu yao.
 Wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu mbele za macho ya Bwana, nao wakamsahau Bwana, Mungu wao, nao wakawatumikia Mabaali na Maashtoreth .Kujiingiza kwa Waisraeli katika ndoa ilikuwa njia tosha ya kuwafunganisha na madhabahu za miungu mingine,kitendo tu cha kuoa au kuolewa yatosha kukuingiza kwenye madhabahu nyingine isipokuwa umepata ufahamu juu ya jambo hilo.
Ndoa ni eneo tosha la kubadili mfumo wako wa maisha kuwa mazuri au mabaya,Israeli waliruhusu mungu baali na maashtoreth kupitia ndoa na kila madhabahu ina Mungu wake na tabia zake.
Suleiman alipooa wanawake wa kigeni walibadili imani yake mbele ya madhabahu ya Mungu(1Wafalme 11.1-8 1 Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti,
  na wa mataifa Bwana aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda.
 Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo.
  Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake.
  Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni.
 Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake.
 Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni.
 Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa nchi za kigeni, waliofukiza uvumba, wakawatolea miungu yao dhabihu.)”You must not intermarry with them because they will surely turn your heart after their gods..hii ni sababu tosha ya kulinda imani yako kwa Kristo ili usije ukaingia katika madhabahu za baali.na kujifunganisha kwa kutoa sadaka.
Tambua kuwa unapoanza agano la ndoa kuna kuwa na mifumo tofauti ya kiutwala katika maisha yako
  Baadhi ya miungu na harakati zake juu ya makabila ya Israel 2Falme 23:13.( Nazo madhabahu zilizokuwako darini juu ya chumba cha juu cha Ahazi, wafalme wa Yuda walizozifanya, nazo madhabahu alizozifanya Manase katika behewa mbili za nyumba ya Bwana, mfalme akazivunja, akazitelemsha huko nje, na kuyatupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni.
 Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, mfalme wa Israeli, kwa Ashtorethi, chukizo la Wasidoni, na Kemoshi, chukizo la Moabu, na Milkomu, chukizo la wana wa Amoni, mfalme akapanajisi.
  Akazivunja-vunja nguzo, akayakata-kata maashera, akapajaza mahali pake mifupa ya watu)
1.   Ashtoreshi – alikuwa mungu mke wa kabila la wasidoni, kama inavyoonekana katika 1 Wafalme 11:33. Ashtoreshi ni kirefu cha “Ashera” ambaye pia aliaminiwa kuwa ni mungu anayefanikisha uzazi wa kila kitu. kwa sababu wameniacha mimi wakaabudu Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni, na Kemoshi, mungu wa Wamoabi, na Milkomu, mungu wa wana wa Amoni wala hawakuenda katika njia zangu, kutenda mema machoni pangu, kuzishika sheria zangu na hukumu zangu, kama Daudi baba yake.

Kemoshi – alikuwa mungu wa wamoabi – mungu kemoshi na baal – peori ni miungu iliyowatesa sana kabila la moabi hata kwa kuwafanya kuwa waasherati na wazinzi – Hesabu 25:1 – 3. Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu;
 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.
 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.
 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.
 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal-peori.
 Na tazama, mtu mmoja miongoni mwa wana wa Israeli akaja na kuwaletea nduguze mwanamke Mmidiani mbele ya macho ya Musa, na mbele ya macho ya mkutano wote wa wana wa Israeli, hapo walipokuwa walia mbele ya mlango wa hema ya kukutania.


3.       Milkomu au moleki – alikuwa mungu wa Amoni. Moleki alilitawala na kulikandamiza kabila la waamoni. Mungu moleki ndiye aliyelifanya kabila la waamoni kuamini kwamba, wakitoa sadaka ya kafara ya watoto watafanikiwa na kuwa karibu na mungu – Lawi 20:1 – 5( Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
  Tena uwaambie wana wa Israeli, Mtu awaye yote miongoni mwa wana wa Israeli, au miongoni mwa wageni waketio katika Israeli, atakayetoa katika kizazi chake na kumpa Moleki, sharti atauawa; wenyeji wa nchi watampiga kwa mawe.
 Mimi nami nitamkazia uso wangu mtu huyo, nami nitamkatilia mbali na watu wake; kwa kuwa ametoa katika kizazi chake na kumpa Moleki, ili kupatia unajisi patakatifu pangu, na kulinajisi jina langu takatifu.
 Tena kama wenyeji wa nchi wakimfumbia macho mtu huyo kwa njia yo yote, hapo atoapo katika kizazi chake na kumpa Moleki, wasimwue;
  ndipo mimi nitamkazia uso wangu mtu huyo, na jamaa zake, nami nitamkatilia mbali, na hao wote wamwandamao katika uzinifu, ili kufanya uzinifu pamoja na Moleki, watengwe mbali na watu wao) 2Falme 17:17 ndiye anayeongoza ibada za sadaka za watoto mpaka leo, na sadaka za mimba changa. Sulemani alipomuoa mke wa Amoni bila kujua miungu ya chimbuko lake, ghafla nafsi yake ilinaswa katika ulimwengu wa giza na akaanza kujenga madhabahu kwa ajili ya mungu Moleki. Na kuanzia hapo miungu 4 ilianza kummiliki – 1Falme 11:5 -7.

 Unaposoma 1Falme 11:3-8” Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo.
  Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake.
 Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni.
 Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake.
 Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni.
 Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa nchi za kigeni, waliofukiza uvumba, wakawatolea miungu yao dhabihu.

-          Unagundua kuwa, nafsi ya Mfalme Sulemani ilifungwa pingu na miungu 4.
Ø Ashtoreshi – mungu mke wa wasidoni
Ø Milkomu au moleki – mungu wa Waamoni
Ø Kemoshi – mungu wa Wamoabu
Ø Baal – miungu ya Wafilisti ambayo aliitolea sadaka.
(7)Jambo la saba.Maagano ya kinadhiri yaliyoweka wakati ukiwa tumboni mwa mama yako au kabla hata ya wewe katika ulimwengu huu wa mwili.Hili ni jambo linine ambalo linatosha kabisa kukufunganisha kabisa na madhabahu Fulani.Wapo wazazi kabla ya wewe kuzaliwa wa huenda wanaipitia eneo gumu la kukupata wewe,wanafikia sehemu ili uzaliwe wanaweka agano la kinadhiri kwa miungu Baali au Mungu aliyehai hivyo kiroho kwa namna moja au nyingine unakuwa umeunganishwa na madhabahu husika kabla yaw ewe kuzaliwa.Nimeona watu wanapata matatizo ambayo yanatokana na madhara ya wao kuunganishwa kwenye madhabahu za miungu baali na maisha yao yanakosa muelekeo kwa sababu uhai wa maisha yao ya badae umefungwa katika madbahahu ya miungu baali.Kadhalika kwa Mungu pia ni hivyo hivyo,Tazama habari za Hana kabla ya Samweli kuzaliwa alikwisha muunganisha na madhabahu ya Mungu(1Samweli  1:11 Then she made a vow and said,O Lord of hosts if you will indeed look on tha afflication of your maidservant and remember me and not forget your maidservant,but will give your maid servant a MALE CHILD then I will give him to the Lord all days of his life and no razor shall come upon his head”)hiyo lilikuwa agano la kinadhiri ambalo ilimsababisha Mungu kumjibu Hana na kuzaliwa kwa mtoto mume Samweli na badae anampeleka madhabahuni kwa kuhani Eli angalia na jina alilompa mwanae,lilikuwa na muunganiko kiroho na agano ambalo aliweka kwenye madhabahu ya Mungu na Mungu anapata nafasi ya kupitisha nguvu zake hapo kwa ajili ya taifa la Israeli(1samweli 1:22) kwa hiyo ni vema sana ukajua namna ya mfumo mzima wa wewe kuzaliwa na kaa na wazazi wako uwaulize habar zako kabla yaw ewe kuzaliwa,wapo wanaotaka wazaliwa wao wa kwanza wamtumikie Mungu na ndio maana unajikuta upo nyumbani mwa Mungu na vita vyake vya rohoni si vya kawaida.



NAMNA GANI UTAJINASUA NA MIUNGU BAALI?

Mruhusu Mungu Akupe maeneo ya kushughulikia kimaombi maana usiende kwa namna unavyofikiri kushulika na madhabahu nyingine maana inahitaji sana nguvu za MUNGU
Hili jambo si la kawaida na si krahisi kwa sababu ya vitu vilivyowekwa na kukuunganisha na madhabahu za miungu baali.Tazama nami Waamuzi 6;25 Maelekezo anayoyapokea Gideon juu ya kuvunja madhabahu za baali amtwae ng’ombe maana yake kuwa sadaka ya Damu kwa agano la kale lakini sasa ipo Damu ya Yesu pekee ya kukutoa katika maagano hayo ya miungu baali yanayoshikilia mfumo mzima wa maisha yako’sasa kila madhabahu inatabia na mifumo yao na Mungu pekee ndie atakayetoa ufahamu na maarifa ya kutoka huko kwenye madhabahu za baali.
Madhabahu zinaweza wakilishwa na vitu mbalimbali mfano miti mikubwa(mwanzo 21;33),kwenye milima(kutoka 3:12 Yohana 4:20)ndio maana yakupasa uombe muongoze kwa Mungu mwenyewe namna ya kutoka huko.
  Upo uhusiano mkubwa sana kati ya maisha yako binafsi na madhabahu husika na kila moja inafumo wake. Angalia madhabahu aliyoibeba Yesu kipindi anazaliwa Je ulishawai kujiuliza kwa nini Herode aliagiza watoto wa miaka miwili tena wakiume wauawe?Ukienda pasipo utaratibu wa Mungu juu ya madhabahu ulioko,kujinasua italetashida isipokuwa kwa njia y Yesu tu
Ndani ya Yesu kulikuwa na mfumo wa kitwala kifalme rohoni na ulimwengu wa nyama
Mifumo miwili ya kiutawala yenye kutofautiana kiitifaki haiwezi kukaa pamoja hata siku moja.

MUNGU AKUBARIKI SANA NA AKUPE UFAHAMU NA UELEWA ZAIDI JUU YA MASUALA MAZIMA YA MADHABAHU
Mwl.Fredrick J Lupenza.







NADHIRI

MAOMBI YA NADHIRI YAAMBATANAYO NA SADAKA YA NADHIRI NENO; Mhubiri 5:4 “ wewe ukimwekea Mungu nadhiri ,usikawie kuiondoa” Maombi...