Sunday, 27 July 2014

JIFUNZE KUWA NA MOYO WA MSAMAHA ILI MUNGU AKUFANIKISHE KIKAMILIFU



Mwawezaje kutembea pamoja mkiwa hamjapatana?
Amosi.3;3
Hili ni swali ambalo  Amosi alikuwa anawambia wana wa Israel na jamaa zao.. fikra kama ndani yenu hamna upendo..na upendo hujengeka ndani ya mtu binafsi na si kwa sababu Fulani..maana upendo wa visababu haudumu.
Amos alisisitiza jambo hili ju ya upendo baina ya ndugu au mtu na mtu.swali juu yako Je mwawezaje kuishi pamoja kama huna moyo wa msamaha?Jambo la kuzingatia…fikra ..mawazo..na mtazamo….zisipoenda pamoja  hakika Baraka za MUNGU  haviwezi zikakaa kwenu..
Yakupasa muishi maisha ya upendo na roho ya msamaha ili Mung afanye makazi ndani yenu maan pasipo kuwa hivyo ni mlangon tosha wa kufunga Baraka za Mungu kwenye maisha yenu au ya mtu binafsi.Malengo ya kimaisha hayawezi kutimia kama ndani yako au yenu hamna moyo wenye upendo na msamaha maana Mungu na Baraka zake zinakaa mahali penye utulivu wa moyo na upatanisho…
Neno kutembea pamoja lina maana ya
  A)upendo halisi ndani yenu au baina yenu.
 B)kuchukuliana na kuwa na fikra patanifu.
 C)pasipo matengano yaani mioyo yenye kunai mamaja pasipo utengano.
kimtazamo neon hili lina maana ya hamwezi mkakaa pamoja na nia na mtazamo na
Jilindeni! Kama ndugu yako akikosa, mwonye. Akitubu msamehe. Na kama akikukosa mara saba katika siku moja na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe
Yesu anatutazamia kuwasamehe waamini wenzetu, wakati wanapotubu. TUnapoomba na kusema, “Utusamehe deni zetu kama nasi tunavyowasamehe wadeni wetu” tunamwomba Mungu atutendee kama ambavyo na sisi tumewatendea wengine. Hatutazamii Yeye atusamehe kama hatutaomba. Basi, mbona sisi tudhani kwamba anatutazamia kuwasamehe wale wasio-omba?
Usimchukie ndugu yako moyoni mwako; ni lazima kumkemea jirani yako, wala usichukue dhambi kwa ajili yake. Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako, bali umpende jirani yako kama nafsi yako. Mimi ndimi BWANA (Walawi 19:17, 18.)
Msamaha ni njia pekee ya watu kuwa pamoja pale wanapokoseana..na hapo ndipo kuna upatanisho
Mahusiano mazuri huachilia mifumo na mitazamo mipya ya kiamafanikio katika maisha,Moyo wa mtu hunawiri palipo na mahusiano mazuri maana hapo ndipo penye tulizo la moyo..(efeso 4;31.mt 5;21) 


Neno la msingi  “Tafuteni kwa bidii kuwa na amanina watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwanaasipokuwa nao.” Waebrania 12:14. Hatuwezi kuwa na amani na watu wote kama hatuna uhusiano mzuri na Mungu. Biblia inatuonyesha mifano ya watu wengi waliokuwa na uhusiano mzuri na Mungu jinsi walivyokuwa na amani na watu wote. Tukianza na Yusufu mwana wa Yakobo, pamoja na kuuzwa utumwani na ndugu zakeambao walikuwa wakimchukia, bado aliendelea kuwa na amani nao pale walipomkuta ni kiongozi mkubwa nchini Misri (Mwanzo 37, 38, 39). Pia tunamuona mtumishi wa Mungu Stefano katikati ya maumivu ya kupigwa na mawe hata kufa bado na yeye alikuwa na amani na watu wale waliokuwa wakimpiga na kuwaombea kwa Mungu asiwahesabie dhambi ile. Hata Bwana wetu Yesu Kristo katikati ya mateso makubwa ya dhihaka na aibu, alipongongomewa msalabani na kuchomwa mkuki ubavuni bado aliendelea kuwa na amani na watu wote naye akawaombea kwa Baba. “Yesu akasema, Baba uwasamehe,kwa kuwa hawajui walitendalo...” Luka 23:34.
Ni maombi yangu kwa Mungu kwamba mimi na wewe  tujifunze na zaidi sana tuwe na uhusiano mzuri na Mungu ili tuwezekuwa na amani na watu wote pamoja na utakatifu na siku moja tumwone
Bwana Mungu mbinguni. Kama viumbe tumeumbwa tuhusiane kwa namna moja au nyingine ili
kufanya dunia iwe sehemu nzuri ya kuishi.Kama wanadamu tunahusiana na watu, vitu, viumbe hai na visivyo hai pamoja na mazingira yanayotuzunguka. Basi uhusiano ni kitu cha muhimu sana kujifunza.

“Wapenzi na tupendane, kwa kuwa pendo latoka kwa mungu; na kila
apendaye amezaliwa na mungu naye anamjua mungu.Yeye asiyependa
hakumjua mungu, kwa maana mungu ni upendo.”
Yohana 4:7-8

Mungu akubariki sana.
  Na mwl.Fredrick J Lupenza

MAOMBI YA NADHIRI YAAMBATANAYO NA SADAKA YA NADHIRI





MAOMBI YA NADHIRI YAAMBATANAYO NA SADAKA YA NADHIRI
NENO;
Mhubiri 5:4 “wewe ukimwekea Mungu nadhiri ,usikawie kuiondoa”
Maombi ya nadhiri ni maombi afanyayo mtu kwa hiari ya moyo wake juu ya jambo Fulani na unaachilia ahadi ndani ya moyo wako ambayo itamsukuma Mungu kujibu maombi yako sawasawa na muda ambao Mungu anatimiza ahadi yako.au
Ni maombi afanyayo mtu kwa hiari yake mwenyewe na Mungu anayemtumkia  kiasi cha majibu yake yamefichwa katika ahadi  ya hiari kati yake na MUNGU ambayo ndio patano lake na MUNGU. Akitafuta sana mwongozo wa Mungu, Yeftha anaweka nadhiri hii kwa Mungu: “Hakika ukiwatia wana wa Amoni mkononi mwangu, itatukia pia kwamba yule atakayetoka nje, atakayetoka nje ya milango ya nyumba yangu kuja kunipokea nitakaporudi kwa amani kutoka kwa wana wa Amoni, lazima atakuwa wa MUNGU, nami nitamtoa huyo kuwa toleo la kuteketezwa.” Waamuzi 11:30-33.
Roho ya Mungu ilikuwa ikitenda juu ya Yeftha alipoweka nadhiri hiyo, na pia MUNGU alibariki jitihada zake. Maandiko yanamsifu Yeftha kwa sababu ya imani yake na kwa yale aliyofanya kuhusiana na kusudi la Mungu. (1 Samweli 12:11; Waebrania 11:32-34)Kwa hiyo, hangefikiria hata kidogo kumtoa mwanadamu awe dhabihu. Kufanya hivyo ni uuaji. Hivyo basi, Yeftha alikuwa akifikiria nini alipoweka nadhiri ya kumtoa mtu kwa MUNGU?NADHIRI ZAKO MBELE ZA MUNGU ZISIZIDI UWEZO WAKO KIIMANI ILI KUTIMIZA
Ni wazi kwamba Yeftha alimaanisha kuwa angemtoa yule ambaye angekuja kumpokea ili amtumikie Mungu kikamili.
Hiyo ni nadhiri ambayo Yeftha aliweka kwa MUNGU..na Mungu akafanikisha..Angalia habari za Yakobo  kaweka nadhiri na ikamsukuma Mungu kujibu (Mwanzo 28;20-22)
USIWEKE NADHIRI MBELE ZA MUNGU KAMA ROHO WA MUNGU HAJAKUSHUHUDIA NDANI YAKO MATOKEO YAKE UTAKUWA NA DENI MBELE ZA MADHABAHU YA MUNGU.
VIPENGELE VYA NADHIRI MBELE ZA MUNGU
A)uwe na hoja yenye nguvu mbele za MUngu  au neon lenye nguvu isaya 41:21
B)uwe na sadaka ya hiari maana sadaka yako ni patano timilifu mbele za MUNGU.Mwanzo 28;20,1Samw.1;10-12
c)uwe na muda  muafaka wa kutoa nadhiri yako iliyobeba maombi yako
d)ukiweka nadhiri yako hakikisha unaitoa na usiweke nadhiri kama ndani yako huna uhakika wa kuitimiza maana ni suala lenye gharama kwako.Kumb.23;21-23,Zab 50.14
e)Usitoe nadhri yako mahali ambapo Mungu hajapatana nawe…kama umwemwaidi Mungu kumtolea eneo Fulani usitoe kinyume na patano lako na Mungu kwa itabaki kuwa deni mbele ya madhabahu ya MUNGU.Mwanzo 31:13,17,hesabu 30;3-16.
kumbuka yapo madhara ya kutotimiza nadhiri yako kwa MUNGU moja wapo ni
Anania na safira waliweka nadhiri yao ya kuuza kiwanja na kukabidhi fedha ila baadaye waliona tamaa na kutoweza kutimiza nadhiri yao, matokeo yake ni kifo.Unaishi katika mashaka na wasiwasi muda wote kwani nadhiri yako hujaitoa kwa Mungu.Matendo ya mitume 5:1-11..Maendeleo ya kiimani na kiuchumi yanadumaa kutokana na kutotimiza nadhiri yako.

Mungu akubariki sana
 Na mwl.Fredrick J Lupenza

KUMWABUDU MUNGU KATIKA UZURI WA UTAKATIFU WAKE

Ni furaha katika kumwabudu Mungu kikamilifu.




Wana wa MUNGU
mtumishi wa MUNGU Joshua Mlelwa katika ibada ya kusifu na kuabudu Mwenge lutherani


NADHIRI

MAOMBI YA NADHIRI YAAMBATANAYO NA SADAKA YA NADHIRI NENO; Mhubiri 5:4 “ wewe ukimwekea Mungu nadhiri ,usikawie kuiondoa” Maombi...