Mwawezaje kutembea
pamoja mkiwa hamjapatana?
Amosi.3;3
Hili ni swali
ambalo Amosi alikuwa anawambia wana wa
Israel na jamaa zao.. fikra kama ndani yenu hamna upendo..na upendo hujengeka
ndani ya mtu binafsi na si kwa sababu Fulani..maana upendo wa visababu haudumu.
Amos alisisitiza jambo
hili ju ya upendo baina ya ndugu au mtu na mtu.swali juu yako Je mwawezaje
kuishi pamoja kama huna moyo wa msamaha?Jambo la kuzingatia…fikra ..mawazo..na
mtazamo….zisipoenda pamoja hakika Baraka
za MUNGU haviwezi zikakaa kwenu..
Yakupasa muishi maisha
ya upendo na roho ya msamaha ili Mung afanye makazi ndani yenu maan pasipo kuwa
hivyo ni mlangon tosha wa kufunga Baraka za Mungu kwenye maisha yenu au ya mtu
binafsi.Malengo ya kimaisha hayawezi kutimia kama ndani yako au yenu hamna moyo
wenye upendo na msamaha maana Mungu na Baraka zake zinakaa mahali penye utulivu
wa moyo na upatanisho…
Neno
kutembea pamoja lina maana ya
A)upendo halisi ndani yenu au baina yenu.
B)kuchukuliana na kuwa na fikra patanifu.
C)pasipo matengano yaani mioyo yenye kunai
mamaja pasipo utengano.
kimtazamo neon hili
lina maana ya hamwezi mkakaa pamoja na nia na mtazamo na
Jilindeni! Kama ndugu
yako akikosa, mwonye. Akitubu msamehe. Na kama akikukosa mara saba
katika siku moja na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe
Yesu anatutazamia
kuwasamehe waamini wenzetu, wakati wanapotubu. TUnapoomba na kusema, “Utusamehe
deni zetu kama nasi tunavyowasamehe wadeni wetu” tunamwomba Mungu atutendee
kama ambavyo na sisi tumewatendea wengine. Hatutazamii Yeye atusamehe kama hatutaomba.
Basi, mbona sisi tudhani kwamba anatutazamia kuwasamehe wale wasio-omba?
Usimchukie ndugu yako
moyoni mwako; ni lazima kumkemea jirani yako, wala usichukue dhambi kwa
ajili yake. Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako,
bali umpende jirani yako kama nafsi yako. Mimi ndimi BWANA (Walawi
19:17, 18.)
Msamaha ni njia pekee
ya watu kuwa pamoja pale wanapokoseana..na hapo ndipo kuna upatanisho
Mahusiano mazuri
huachilia mifumo na mitazamo mipya ya kiamafanikio katika maisha,Moyo wa mtu
hunawiri palipo na mahusiano mazuri maana hapo ndipo penye tulizo la moyo..(efeso
4;31.mt 5;21)
Neno la msingi “Tafuteni kwa bidii kuwa na amanina watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwanaasipokuwa nao.” Waebrania 12:14.
Hatuwezi kuwa na amani na watu wote kama hatuna uhusiano mzuri na Mungu.
Biblia inatuonyesha mifano ya watu wengi waliokuwa na uhusiano mzuri na
Mungu jinsi walivyokuwa na amani na watu wote. Tukianza na Yusufu mwana
wa Yakobo, pamoja na kuuzwa utumwani na ndugu zakeambao walikuwa
wakimchukia, bado aliendelea kuwa na amani nao pale walipomkuta ni
kiongozi mkubwa nchini Misri (Mwanzo 37, 38, 39). Pia tunamuona mtumishi
wa Mungu Stefano katikati ya maumivu ya kupigwa na mawe hata kufa bado
na yeye alikuwa na amani na watu wale waliokuwa wakimpiga na kuwaombea
kwa Mungu asiwahesabie dhambi ile. Hata Bwana wetu Yesu Kristo katikati
ya mateso makubwa ya dhihaka na aibu, alipongongomewa msalabani na
kuchomwa mkuki ubavuni bado aliendelea kuwa na amani na watu wote naye
akawaombea kwa Baba. “Yesu akasema, Baba uwasamehe,kwa kuwa hawajui walitendalo...” Luka 23:34.
Ni maombi yangu kwa Mungu kwamba mimi na wewe
tujifunze na zaidi sana tuwe na uhusiano mzuri na Mungu ili tuwezekuwa
na amani na watu wote pamoja na utakatifu na siku moja tumwone
Bwana Mungu mbinguni. Kama viumbe tumeumbwa tuhusiane kwa namna moja au nyingine ili
kufanya dunia iwe sehemu nzuri ya kuishi.Kama wanadamu tunahusiana na watu, vitu, viumbe hai na visivyo hai pamoja na mazingira yanayotuzunguka. Basi uhusiano ni kitu cha muhimu sana kujifunza.
Bwana Mungu mbinguni. Kama viumbe tumeumbwa tuhusiane kwa namna moja au nyingine ili
kufanya dunia iwe sehemu nzuri ya kuishi.Kama wanadamu tunahusiana na watu, vitu, viumbe hai na visivyo hai pamoja na mazingira yanayotuzunguka. Basi uhusiano ni kitu cha muhimu sana kujifunza.
“Wapenzi na tupendane, kwa kuwa pendo latoka kwa mungu; na kila
apendaye amezaliwa na mungu naye anamjua mungu.Yeye asiyependa
hakumjua mungu, kwa maana mungu ni upendo.”
Yohana 4:7-8
Mungu akubariki sana.
Na mwl.Fredrick J Lupenza