Friday, 1 December 2017

MISINGI KADHAA YA KUKUPA UFAHAMU ANGALU UJUE NAMNA YA KUMALIZIA JAMBO ULILONALO AU WAZO LILILOKO NDANI YAKO KWA NAMNA YA KIMUNGU





Mithali 24:10
“UKIZIMIA SIKU YA TAABU, NGUVU ZAKO NI CHACHE”

  1. Msingi wa Kwanza

         Tambua utendaji wa malaika wa Bwana katika eneo la kukutia nguvu ya Kumaliza kazi uliyoianzisha au jambo
       Tazama hapa Luka 22:42-43 “Ee Baba ikiwa ni mapenzi yako uniondolee kikombe (kazi aliyokuwa amekwisha ianza Yesu ya kuelekea msalabani) hiki walakini si mapenzi yangu bali mapenzi yako yatendeke 43.Malaika mbinguni akamtokea, AKAMTIA NGUVU”
       Na katika hilo jambo lako “Jiulize kama ni mapenzi ya Baba aliye mbinguni au la kwako”! kwa sababu hiyo utagundua kuwa “kuna mvutano wa ndani kati ya Roho yako na Mwili wako kati kati ya nafsi yako inayo katibu habari kati ya mwili na roho yako” Kwa kuwa roho I radhi lakini mwili ni dhaifu
Kutoka 23:20,23,
 “Tazama , mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani(Akutie nguvu ya kumaliza jambo si tu kukulinda) na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengenezea 23.Kwa kuwa malaika wangu atatangulia mbele yako na kukufikisha kwenye Mwamori, na mhiti, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi nami nitawakatilia mbali”(Soma pia na Kutoka 23:27-30, Ebrania 1:14, Zab 91:11, 34:7-8)
       Tazama pia habari za Petro gerezani “alikaa gerezani akiwa amefungwa minyororo pamoja na walizi wa kumlinda walikuwepo lakini kwa maombi ya kanisa bila kukoma ikamsukuma Mungu kutuma Malaika wake Kumtetea kwa sababu kazi ilikuwa bado hajaimaliza” (Mdo 12:5-10), kwa mantiki hiyo Jifunze pia kusukuma jambo lako kwa namna ya Maombi ambayo yanaachilia utendaji wa Mungu kwenye hilo jambo na kulikamilisha hakika (ukimwita Mungu kila wakati, palipo na ugumu huingilia kati na kufanya wepesi katika hilo jambo ambalo umelianzisha)

Mungu Akubariki sana..Itaendelea Msingi wa Pili..

NADHIRI

MAOMBI YA NADHIRI YAAMBATANAYO NA SADAKA YA NADHIRI NENO; Mhubiri 5:4 “ wewe ukimwekea Mungu nadhiri ,usikawie kuiondoa” Maombi...