MAOMBI YA
NADHIRI YAAMBATANAYO NA SADAKA YA NADHIRI
NENO;
Mhubiri 5:4
“wewe ukimwekea Mungu nadhiri
,usikawie kuiondoa”
Maombi ya nadhiri ni maombi afanyayo mtu kwa hiari ya moyo wake
juu ya jambo Fulani na unaachilia ahadi ndani ya moyo wako ambayo itamsukuma
Mungu kujibu maombi yako sawasawa na muda ambao Mungu anatimiza ahadi yako.au
Ni maombi
afanyayo mtu kwa hiari yake mwenyewe na Mungu anayemtumkia kiasi cha majibu yake yamefichwa katika
ahadi ya hiari kati yake na MUNGU ambayo
ndio patano lake na MUNGU. Akitafuta sana mwongozo wa Mungu, Yeftha anaweka
nadhiri hii kwa Mungu: “Hakika ukiwatia wana wa Amoni mkononi mwangu, itatukia
pia kwamba yule atakayetoka nje, atakayetoka nje ya milango ya nyumba yangu
kuja kunipokea nitakaporudi kwa amani kutoka kwa wana wa Amoni, lazima atakuwa
wa MUNGU, nami nitamtoa huyo kuwa toleo la kuteketezwa.” Waamuzi 11:30-33.
Roho
ya Mungu ilikuwa ikitenda juu ya Yeftha alipoweka nadhiri hiyo, na pia MUNGU
alibariki jitihada zake. Maandiko yanamsifu Yeftha kwa sababu ya imani yake na
kwa yale aliyofanya kuhusiana na kusudi la Mungu. (1 Samweli
12:11; Waebrania
11:32-34)Kwa hiyo,
hangefikiria hata kidogo kumtoa mwanadamu awe dhabihu. Kufanya hivyo ni uuaji.
Hivyo basi, Yeftha alikuwa akifikiria nini alipoweka nadhiri ya kumtoa mtu kwa
MUNGU?NADHIRI ZAKO MBELE ZA MUNGU ZISIZIDI UWEZO WAKO KIIMANI ILI KUTIMIZA
Ni wazi kwamba Yeftha alimaanisha
kuwa angemtoa yule ambaye angekuja kumpokea ili amtumikie Mungu kikamili.
Hiyo ni nadhiri ambayo Yeftha
aliweka kwa MUNGU..na Mungu akafanikisha..Angalia habari za Yakobo kaweka nadhiri na ikamsukuma Mungu kujibu (Mwanzo
28;20-22)
USIWEKE
NADHIRI MBELE ZA MUNGU KAMA ROHO WA MUNGU HAJAKUSHUHUDIA NDANI YAKO MATOKEO
YAKE UTAKUWA NA DENI MBELE ZA MADHABAHU YA MUNGU.
VIPENGELE
VYA NADHIRI MBELE ZA MUNGU
A)uwe
na hoja yenye nguvu mbele za MUngu au
neon lenye nguvu isaya 41:21
B)uwe
na sadaka ya hiari maana sadaka yako ni patano timilifu mbele za MUNGU.Mwanzo
28;20,1Samw.1;10-12
c)uwe
na muda muafaka wa kutoa nadhiri yako
iliyobeba maombi yako
d)ukiweka
nadhiri yako hakikisha unaitoa na usiweke nadhiri kama ndani yako huna uhakika
wa kuitimiza maana ni suala lenye gharama kwako.Kumb.23;21-23,Zab 50.14
e)Usitoe
nadhri yako mahali ambapo Mungu hajapatana nawe…kama umwemwaidi Mungu kumtolea
eneo Fulani usitoe kinyume na patano lako na Mungu kwa itabaki kuwa deni mbele
ya madhabahu ya MUNGU.Mwanzo 31:13,17,hesabu 30;3-16.
kumbuka yapo madhara ya kutotimiza nadhiri yako kwa MUNGU moja wapo ni
Anania na safira waliweka nadhiri yao ya kuuza kiwanja na kukabidhi fedha ila baadaye waliona tamaa na kutoweza kutimiza nadhiri yao, matokeo yake ni kifo.Unaishi katika mashaka na wasiwasi muda wote kwani nadhiri yako hujaitoa kwa Mungu.Matendo ya mitume 5:1-11..Maendeleo ya kiimani na kiuchumi yanadumaa kutokana na kutotimiza nadhiri yako.
Mungu akubariki sana
kumbuka yapo madhara ya kutotimiza nadhiri yako kwa MUNGU moja wapo ni
Anania na safira waliweka nadhiri yao ya kuuza kiwanja na kukabidhi fedha ila baadaye waliona tamaa na kutoweza kutimiza nadhiri yao, matokeo yake ni kifo.Unaishi katika mashaka na wasiwasi muda wote kwani nadhiri yako hujaitoa kwa Mungu.Matendo ya mitume 5:1-11..Maendeleo ya kiimani na kiuchumi yanadumaa kutokana na kutotimiza nadhiri yako.
Mungu akubariki sana
Na mwl.Fredrick J Lupenza